Back to top

Mpango “Serikali imejipanga kuinua uchumi wa Taifa”

12 June 2021
Share

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt Philip Isdor Mpango, amesema serikali imejipanga kikamilifu katika kusimamia maadili, uawajibikaji na utawala wa sheria katika kuinua uchumi wa viwanda kwa maendeleo ya watu kama ilivyoelekezwa katika mpango wa tatu wa maendeleo ya  taifa wa miaka mitano.

Makamu wa Rais ameyasema hayo jijini Dodoma wakati wa ufunguzi wa mkutano wa nne wa mtandao wa  maombi ya  asubuhi ya kitaifa na kimataifa na kusema kuwa serikali itaendelea kushirikiana na viongozi wa dini katika kuhakikisha kuwa Taifa linakuwa na ustawi bora kwa watu wake.

Aidha Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Rais Dkt Philip Mpango, ameeleza kuwa maombi hayo ni kiunganisho baina ya wanadamu na Mungu wao na kama watoto wa Mungu katika Kupendana na kuwajibika katika kuwatumikia watu wake.