
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Nnauye ameziagiza kampuni za simu nchini kuacha mara moja tabia ya kutuma ujumbe (SMS) ambao haujaombwa na Mteja kwani kufanya hivyo ni kuwapotezea muda na ni usumbufu kwa wateja huku akiielekeza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kushirikiana na kampuni za simu kusimamia agizo hilo.
