Back to top

Mtoto afanyiwa ukatili baada ya kujisaidia kitandani.

16 January 2020
Share


Baba adaiwa kumuua kikatili mwanae kwa kumuunguza na moto sehemu mbalimbali za mwili  kwa kile kinachodaiwa mtoto kuyo alijisaidia kitandani usiku huko wilayani Ngara mkoani Kagera.

Kamanda wa polisi wa Kagera Revocatus Malimi amesema mtoto Bahati Juma mwenye umri wa miaka miwili alipoteza maisha wakati akikimbizwa hospitali na wasamalia wema na jeshi hilo linamshikilia mtuhumiwa Juma Daniel.