Watu wawili wamepoteza maisha katika matukio mawili tofauti yaliyotokea mkoani Arusha likiwemo la mama aliyekatwa panga na mwanaye na tukio la pili likitokana na ajali ya moto.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Arusha Jonathan Shana anaelezea jinsi tukio la mauaji lilivyotokea katika kijiji cha Sakila chini wilayani Arumeru ambapo mama mmoja aliyetajwa kwa jina la Eliyamulika Emanuel Sarakikya (79) ameuawa kwa kukatwa na shoka na mtoto wake aliyetajwa kwa jina la Bw.Daniel Emanuel.
Kamanda Shana pia akaelezea tukio la moto lilitokea eneo la Sanawari katika kata ya Sekei jijini Arusha usiku wa kuamkia 16/05/2020 baada ya duka la bidhaa mbali mbali kuteketea kwa moto huku kijana huyo akiwa ndani amelala.