Mtoto wa kike wa miaka 12 Milembe Maduhu amekutwa ameuawa kwenye nyumba ambayo haijakamilika katika kijiji cha Lamadi kitongoji cha Lamadi wilayani Busega mkoani Simiyu,ambapo watu 3 wanashikiliwa kwa mahojiano.
Chanzo cha mauaji bado hazijafahamika huku Mkuu wa wilaya ya Busega Tano Mwera akiwasihi wakazi wa Lamadi kutulia wakati polisi wakiendelea na uchunguzi wa tukio hilo.