Back to top

Muuguzi wa hospitali ya Mount Meru asimamishwa kazi kwa ulevi.

08 February 2019
Share

Baraza la uuguzi na ukunga nchini limemsimamisha  kazi muuguzi wa hospitali ya Mount Meru Bwana Martin Chamani  kwa kipindi cha mwaka mmoja kwa kosa la kuingia kazini akiwa amelewa kinyume na maadili na kanuni za utumishi.

Akizungumza jijini Arusha Mwenyekiti wa baraza hilo  Abner Mathube anasema licha ya kukiuka maadili ya taaluma ya uuguzi, ulevi kazini unahatarisha maisha ya wagonjwa.