Back to top

Mvua yaua watano na kuharibu mazao Serengeti.

07 February 2020
Share

Watu watano wamekufa huku kaya  zaidi ya  kaya 400 kata ya Kisaka wilaya ya Serengeti zikihofia kukubwa na tatizo  la ukosefu wa chakula kutokana na mazao yao kusombwa na maji kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha mkoa wa Mara.

ITV imefunga safari hadi eneo la tukio na kushuhudia mazao yakiwa yameharibiwa na  baadhi ya wananchi wakiosha na kuanika mazao yaliyosalia hususani mahindi.

Hata hivyo Mkuu wa wilaya ya Serengeti ,Nurdini Babu amesema mbali na kuharibiwa kwa mazao pia mvua hizo zimesababisha vifo vya watu watano  ambao wamekufa baada ya kusombwa na maji huku akidai  serikali inafanya tathimini ili kujua ni hekari ngapi za mazao zimeathirika.