
Wananchi wa eneo la Mwatulole lililopo Kata ya Buhalahala mkoani Geita wamefunga barabara kwa mawe wakiitaka serikali kuweka matuta na alama za zebra kwenye eneo hilo baada ya Mwanafunzi wa shule ya msingi Nguzo Mbili aliyejulikana kwa jina la John Frank (7) darasa la kwanza kugongwa na lori na kufariki palepale wakati akivuka barabara kuelekea shuleni.
