Back to top

Polisi yamshikilia mmoja kwa uchochezi mtandaoni

10 April 2018
Share


Jeshi la Polisi mkoani Lindi, linamshikilia mfanyabiashara Elishi Magoma, mkazi wa wilaya ya Liwale, mkoani Lindi, kwa  kosa la kuhamasisha vurugu na uchochezi kwa njia ya Mtandao.

Kaimu kamanda wa Polisi, mkoa wa Lindi,Renatusi Ngasa,amesema mtuhumiwa  alituma sauti  katika kundi la Telegram Lindi, makala fupi yenye kauli za uchochezi.