Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Magufuli amemsamehe Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Rufiji Brighton Eliud Kilimba aliyetoa taarifa za uongo juu ya ubovu wa gari la kubebea wagonjwa kituo cha afya Ikwiriri Rufiji na sasa yupo huru licha ya taratibu za kumfikisha mahakamani kuwa zilikwishakamilika.
Kamanda wa polisi mkoa wa Kipolisi Rufiji Kamishna Msaidizi Onesmo Lyanga amethibitisha kutolewa kwa msamaha huo kutoka kwa. Mh rais .
Mapema Julai 30 mwaka huu majira ya saa 9 mchana Rais Magufuli akitokea kijijini Lupaso wilayani Masasi mkoani Mtwara katika maziko ya aliyekuwa rais wa awamu ya tatu aliposimama Ikwiriri Rufiji mkoani Pwani kusikikiza kero mbalimbali inadaiwa Bw. Kilimba alitoa taarifa za uongo kwa Mhe rais kuwa gari la kubebea wagonjwa ni bovu liko gereji na linahitaji gharama kubwa za matengenezo wakati anajua sio kweli.