Back to top

Rais Samia awataka Watanzania kuungana katika Sensa.

14 September 2021
Share

Rais wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuungana katika Sensa ya Watu na Makazi na kusema kuwa sensa ijayo itakuwa na mabadiliko tofauti na za miaka iliyopita.
.
Amesema kutakuwa na ongezeko la dodoso la idadi ya majengo nchi nzima hali itakayosaidia kurahisisha ukusanyaji wa kodi.
.
Rais Samia ameyasema hayo Jijini Dodoma kwenye uzinduzi wa mkakati wa uelimishaji na ushirikishwaji wa Sensa ya Watu na Makazi mwaka ujao.
.
Ameitaka kamati ya taifa ya sensa kuwekeza katika kuhamasisha wananchi kujitokeza kuhesabiwa.
.
Kwa upande wake Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi Tanzania Bara, Mhe.Anne Makinda amesema sensa hiyo ni shirikishi na inaanzia ngazi ya kitongoji na kuwataka Watanzania kuona fahari kuhesabiwa.