
Kocha Mkuu wa timu ya Simba SC, Roberto Oliveira 'Robertinho', ameondoka nchini Uturuki ambapo timu hiyo, ipo kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao, na kuelekea nchini Brazil, kwa ajili kuhudhuria kozi fupi ya masomo ya ukocha (FIFA Pro License) yanayofanyika Brazil.
.
Taarifa hiyo imetolewa na timu hiyo ambapo imebainisha kuwa Robertinho atakuwa Brazil kwa muda wa wiki moja na atarejea Uturuki Julai 24, 2023, baada ya mafunzo hayo kumalizika.
