Back to top

Serikali kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji wazalendo na wageni

17 July 2018
Share

Waziri wa nchi sera,ajira, uratibu na Bunge Mheshimiwa Jenista Mhagama amesema kuwa serikali itaendelea kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji wazalendo na wageni ili kuinua uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla.

Ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi katika kijiji cha Maniamba wilayani Songea mkoani Ruvuma  katika mkutano wa hadhara  uliouhuduriwa na mwekazaji kutoka China na mwekezaji wa kampuni ya kizalendo  ya Kamba's Group inayochimba makaa ya Mawe katika kijiji hicho.

Katika mkutano huo kampuni ya Kamba's Group imetoa  Bati,Nondo,Misumari na Saruji kwa ajili ya kukamilisha ofisi ya kijiji cha Maniamba ambapo kwa sasa wanatumia jengo la  mashine ya kusaga nafaka kama ofisi.