Serikali imeifunga kwa muda usiojulikana Shule ya Msingi Nyamkazi iliyoko katika ya Manispaa ya Bukoba baada ya kuzingirwa na maji yaliyotokana na mvua zinazoendelea kunyesha kwenye maeneo mbalimbali mkoani Kagera na hivyo kusababishwa mafuriko kutokana na ongezeko la maji katika Ziwa Victoria.
Uamzi wa kufunga shule umefanywa siku mbili baada ya Mkuu wa Wilaya ya Bukoba, Deodatus Kinawiro kutoa mapendekezo kwa madiwani ya kufanya mchakato kutafuta eneo jipya la ujenzi wa shule hiyo ili walinde usalama wa wanafunzi.