Back to top

Serikali yanunua rada 3,kufungwa Mtwara, Mbeya na Kigoma.

23 March 2020
Share

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe amesema katika kuboresha huduma za hali ya hewa  nchini Serikali imenunua rada tatu ambazo zitafungwa katika  mikoa ya Mtwara, Mbeya na Kigoma.
 
Akizungumza  jijini Dodoma ikiwa ni kilele cha Maadhimisho ya  siku ya hali hewa Duniani  katika ofisi za Mamlaka ya hali ya hewa nchini (TMA)  Mhandisi Kamwelwe alisema, baada ya kufungwa rada hizo kutakuwa na mtandao wenye jumla ya Rada tano ambazo zitakuwa na uwezo wa kuliona anga la Tanzania kwa asilimia 70.