Back to top

Shule ya Msingi Mnyonga yakabiliwa na upungufu wa Madawati

15 April 2018
Share

Shule  ya msingi  Mnyonga ambayo  ni ya mchanganyiko pamoja wanafunzi wenye Ulemavu iliyoko Peramiho mkoani Ruvuma inakabiliwa na changamoto mbalimbali  ikiwemo upungufu wa  madarasa ambapo kati ya madarasa kumi na mbili yanayotakiwa kwasasa ina madarasa manne tu.

Changamoto hizo zimeelezwa na Mwalimu Mkuu Msaidizi  wa shule hiyo Mwalimu Monica Kasia  ambapo amesema kuwa shule hiyo pia ina upungufu wa Madawati wanafunzi wanakaa chini, ukosefu wa Bwalo la kulia hivyo wanafunzi hula wakiwa wameketi kwenye Nyasi  na pia haina  Jiko na hivyo Mpishi hupika akainyeshewa na mvua.

Kutokana na  changamoto hiyo jumuiya ya wazazi ya Chama Cha Mapinduzi Songea vijijini imetoa  misaada mbalimbali  kupunguza baadhi yachangamoto zinazoikabili shule hiyo.