Back to top

Simba na Yanga sio timu za kugombania Ligi Kuu pekee

16 April 2022
Share

Mfadhili wa zamani wa Simba Mzee Azim Dewji amesema kuwa Simba na Yanga sio timu za kugombania Ligi Kuu Bara pekee bali Ligi hiyo iwe ni kikanyagio tu cha kwenda kucheza mashindano ya wakubwa mfano CAF ambapo amewakaribisha timu hiyo pinzani kuja kushuhudia mechi ya wakubwa dhidi ya Orlando Pirates huku akisisitiza kuwa watafurahi ingawa moyoni wanaweza wakaumia ila wataona mpira utakaotandawaza siku hiyo.