Back to top

TAKUKURU yaokoa milioni 27 walizokuwa wametapeliwa wastaafu.

22 October 2020
Share

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Shinyanga imeokoa na kuzirejesha shilingi milioni ishirini na saba ambazo ni sehemu ya fedha za wastaafu wa umma walizotapeliwa kupitia mikopo umiza, zikiwemo shilingi milioni kumi na laki nne za mwananchi mmoja aliyetapeliwa na Kamishna Msaidizi wa Ardhi kwa lengo la kupimiwa ardhi.

Mkuu wa TAKUKURU mkoani Shinyanga Hussein Mussa wakati amesema hayo wakati akitoa taarifa ya utendaji wa taasisi hiyo mkoani humo katika kipindi cha miezi mitatu.

Wakizungumzia kitendo hicho baadhi ya wastaafu waliotapeliwa wameishukuru taasisi hiyo kwa kufanikisha upatikanaji wa fedha zao walizotapeliwa.