Back to top

TANESCO: KUNA HITILAFU KWENYE GRIDI YA TAIFA

01 April 2024
Share

Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), limesema kumetokea hitilafu kwenye mfumo wa njia ya kusafirisha umeme ya Gridi ya Taifa, hali ambayo imesababisha baadhi ya maeneo nchini kukosa huduma ya umeme.
.
Kupitia taarifa iliyotolewa na Shirika hilo imeeleza kuwa hitilafu hiyo imetokea majira ya Saa 8:22 Usiku, na kwamba wataalamu wake wanaendelea na jitihada za kurejesha huduma hiyo.