Back to top

Tanzania yapata msaada wa dola za Marekani mil.90 kwa ajili ya elimu.

15 January 2020
Share

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepokea msaada wa Dola za Marekani milioni 90 sawa na shilingi bilioni 240.95 kutoka Mfuko wa Ushirikiano wa Elimu Duniani (GPE), kwa ajili ya kugharamia miradi miwili ya Sekta ya Elimu.

Mikataba ya msaada huo imesainiwa katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango jijini Dar es Salaam, na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Doto James kwa upande wa Serikali na Balozi wa Sweden nchini, Bw. Anders Sjoberg, ambaye nchi yake ni Wakala wa Msaada huo kupitia Shirika la Maendeleo la Kimataifa la nchi hiyo (SIDA).


Akizungumza katika hafla ya utiaji saini mikataba ya msaada huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James alisema msaada huo ni kwa ajili ya kugharamia miradi ya Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Elimu (ESDP) 2016/17 – 2021/22  na nyongeza ya Mpango wa Elimu kwa Matokeo (EP4R).