
Mamlaka ya usimamizi wa wanyamapori Tanzania (TAWA) imeendesha msako mkali wa kuwasaka Chui wanaoleta hofu na taharuki kwa wananchi wilayani Mbinga mkoani Ruvuma kwa kuua kondoo 40,mbuzi 22 na ngo'mbe wawili hadi sasa.
Kwa upande wake kaimu afisa mtendaji wa kata ya Ruanda Bw.Elgius Ndimbo anawataka wananchi kufungia mifugo yao kwenye mazizi badala ya kuiacha ikizurula ovyo maporini na kwamba kata hiyo imepakana na mapori ya akiba ya Litumbandyosi na Liparamba ambako chui wanatokea.