Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) imetoa Utabiri wa mwelekeo wa mvua za msimu kwa kipindi cha kuanzia mwezi Novemba mwaka huu hadi mwezi Aprili mwakani ambapo imesema mvua zitaanza kunyesha wiki ya pili ya mwezi Novemba na Utabiri unaonesha uwepo wa mvua za wastani hadi juu ya wastani katika maeneo mengi ya nchi.
Akitoa utabiri huo Jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dk Agness Kijazi amesema viashiria vinaonesha kuwa mvua itanyesha kwa kiwango kizuri .