Back to top

Trump aigomea Iraq,ataka Marekani ilipwe kwanza.

06 January 2020
Share

Rais wa Marekani, Donald Trump, ametishia kuiwekea Iraq vikwazo baada ya bunge la nchi hiyo kupiga kura kupitisha azimio linalovitaka vikosi vya Marekani viondoke nchini humo.

 Trump amesema iwapo wanajeshi hao wataondoka, Iraq itapaswa kuilipa Marekani gharama za kambi ya jeshi la anga iliyoko Iraq. 

Trump amebainisha kuwa hawatoondoka hadi hapo Iraq itakapoilipa Marekani gharama za kambi hiyo ambayo amesema iko muda mrefu hata kabla ya wakati wake na iligharimu mabilioni ya dola kuijenga.