
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, ameagiza wakandarasi nchini kulipa watumishi wao kwa mujibu wa sheria za nchi na si kuwapunja.
Waziri huyo ametoa maelekezo kayo jana wakati akikagua maendeleo ya barabara ya Same- Kisiwani- Mkomazi yenye urefu wa kilometa 100.5 ambayo inajengwa na mkandarasi M/S China Communication Construction Companya Ltd.
Katika tukio hilo alipata malalamiko kuwa wafanyakazi kwenye ujenzi wanalipwa fedha kidogo kuliko kile kinachokubalika kisheria.
“Hii haikubaliki. Kuna viwango ambavyo tumekubaliana kwa mujibu wa sheria zetu. Ni lazima wakandarasi wote wafuate viwango hivyo. Hilo halina mjadala,” alisema Ulega huku akishangiliwa na wafanyakazi hao.
