Back to top

Vijana wanaokwepa mafunzo JKT kuchukuliwa hatua.

15 September 2021
Share

Serikali imeombwa kuwachukulia hatua za kinidhamu vijana wanaokwepa kujiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa mujibu wa sheria kwani kufanya hivyo ni kukaidi utaratibu uliowekwa na serikali.
.
Hayo yamesemwa katika ufungaji wa mafunzo ya vijana wa mujibu wa sheria katika kikosi cha 841 mafinga ambako vijana hao wamesema   mafunzo ya yamewasaidia.
.
Kanali Issa Chalamila ni mkuu wa kikosi cha jeshi hilo la 841 Mafinga na Saad Mtambule mkuu wa wilaya ya Mufindi wamesema lazima mafunzo hayo yapewe kipaumbele.
.
Jumla ya vijana 1443 wa mujibu wa sheria operesheni Samia Suluhu 2021 wamehitimu mafunzo ya awali ya kijeshi katika kambi ya jeshi (JKT) Mafinga