Back to top

VIPAUMBELE VITANO BAJETI YA WIZARA YA ELIMU 2024/2025

08 May 2024
Share

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania laidhinisha zaidi ya shilingi Trilioni 1.97 zilizoombwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa ajili ya kutekeleza vipaumbele vitano vya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 ili kuleta mageuzi ya Elimu nchini.

1. Kuendelea na utekelezaji wa sera na mitaala, mapitio ya sheria na kuandaa miongozo ya utoaji elimu na mafunzo nchini.

2. Kuongeza fursa na kuimarisha ubora wa elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi (amali na amali sanifu).

3. Kuongeza fursa na kuimarisha ubora wa elimu ya msingi, sekondari na ualimu. 

4. Kuongeza fursa na kuimarisha ubora wa elimu ya juu na kuendeleza tafiti, matumizi ya sayansi, teknolojia na ubunifu.

5. Kuendelea na utekelezaji wa Sera na Mitaala, Mapitio ya Sheria na kuandaa Miongozo ya Utoaji Elimu na Mafunzo Nchini.

Wizara ya Elimu imesema kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 wataweka mkazo kwenye Elimu ya Ujuzi (Skillis Oriented) ili kuwawezesha wahitimu wa ngazi mbalimbali za Elimu kujiajiri na kuajiri wengine.