Vyama vitatu vya vya msingivya ushirika( AMCOS) vya Mtiti,Mruji na Sama vimenunua magari kila chama gari moja ili kutatua changamoto ya kusafirisha mazao iliyokuwa ikivikabili vyama hivyo.
Mwandishi wa Mruji (AMCOS) Bw. Zuberi Chiwale amesema kuwa magari hayo yaliyotumika yote matatu yamenunuliwa kwa shilingi milioni 135 za mapato ya ndani ya vyama hivyo.
Kwa upande wake mrajisi msaidizi wa vyama vya ushirika wa mkoa wa Ruvuma Bi.Bumi Masuba amesema ununuzi wa magari hayo ni mwelekeo mzuri wa kukuza uchumi wa vyama hivyo.
Akizindua magari hayo mkuu wa wilaya ya Tunduru Bw.Julius Mtatiro amepongeza hatua hiyo kubwa ya maendeleo na kusema unaviweka vyama vya ushirika kwenye mwelekeo mzuri.