
Baadhi ya Waendesha bodaboda nchini Kenya wameishtaki serikali ya nchi hiyo wakidai kuwa imewaacha nje ya mipango yake, huku wakibainisha kuwa wakati Kenya Kwanza ikiendesha kampeni zake katika uchaguzi uliofanyika mwaka 2022, ilijikita zaidi katika sera za uwezeshaji na kuinua maisha ya watu wanaofanya biashara ya boda boda na Mama Mboga, hali ambayo imekuwa tofauti na sasa.
.
Waendesha bodaboda hao wamesema kuwa sera za Kenya Kwanza, kwa sasa zinawanyima mapato hali inayosabaisha wao kutokuwa na imani na Serikali hiyo. #via #citizendigitalKenya
