Wafanyabiashara wagoma kununua maembe Tanga.

Baadhi ya wafanyabiashara wa maembe kutoka Jijini Dar es Salaam wamegoma kununua maembe ya wakulima wa Kwediboma wilayani Kilindi mkoani Tanga wakidai kuwa ushuru shilingi 300,000/= wanaotozwa na Halmashauri ya Wilaya hiyo kwa gari moja aina ya Fuso ni mkubwa kwao hali iliyopelekea maembe kuozea shambani na kuwaathiri zaidi wakulima.