Back to top

WAGANGA WAFAWIDHI ACHENI KUFANYA KAZI KWA MAZOEA - MOLLEL

18 November 2023
Share

Waganga wafawidhi wa Hospitali zote nchini, wametakiwa kuwajibika na kuacha  kufanya  kazi kwa mazoea, ili kuleta  tija  ya  uwekezaji uliofanywa  na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan, katika sekta ya afya.
.
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel, alipofanya ziara katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, kuangalia hali ya utoaji huduma za afya na kufanya mazungumzo na Wakuu wa Taasisi za Afya, ikiwemo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Taasisi ya Mifupa (MOI), Bohari ya Dawa (MSD), Shirika la Bima la Taifa (NHIF), Mamlaka ya Dawa na Vifaa tiba (TMDA), Mganga Mkuu wa Mkoa  na Waganga Wafawidhi  wa Hospitali za Rufaa za Mkoa wa Dar es saalam.
.
Dkt. Mollel amesisitiza kuwa, Serikali haitamvumilia Kiongozi yoyote anayekwamisha juhudi za uboreshaji wa huduma katika sekta ya afya nchini kwani Rais Samia Suluhu Hassan amefanya mapinduzi makubwa katika sekta ya afya hivyo ni jukumu la usimamizi imara, ili kuleta ubora wa Huduma kwa wananchi.