Back to top

Wanafunzi maarufu ‘mboga 7’ wadaiwa kujihusisha na biashara ya ngono.

15 January 2020
Share

Baadhi ya wanafunzi wanosoma katika shule za kata wilaya ya Musoma mkoa wa Mara wanadaiwa kujihusisha na biashara ya ngono kwenye Club  nyakati za usiku  huku wakijiita majina ya ‘mboga saba’ na ‘sex dadazi’.

 Hayo yamebainishwa na  na Mkuu wa wilaya ya Musoma Vicent Naano wakati akizungumza na wazazi  kwa nyakati tofauti katika shule ya sekondari  Nyabisare na Morembe  ambazo wanafunzi wake  69 wamepata sifuri  kati ya wanafunzi wanafunzi 217 waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka jana.

 Akizungumza na ITV ofisini kwake ofisa elimu sekondari wilaya ya Musoma amekiri kuwepo kwa wanafunzi wanaofanya biashara ya ngono na kudai hali hiyo pia imesababisha matokeo ya kidato cha nne kubwa mabaya ambapo wilaya ya Musoma imeshika nafasi ya  139 kati ya halmashauri 185 kitafa.