Jeshi la Polisi Kitengo cha Dawati la Jinsia na Watoto wilayani Njombe, limetoa elimu ya ukatili wa kingono kwa wanafunzi wa kike wa shule za sekondari wilayani humo.
.
Elimu hiyo imetolewa katika kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia lililowakutanisha wanafunzi wa kike kutoka shule 5 za serikali zilizopo mjini Njombe, lililoandaliwa na Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi (UWT).