Back to top

Wananchi Mara waomba bweni kunusuru watoto wasiuawe na tembo na simba.

27 June 2020
Share

Wananchi wa vijiji  vinne vilivyopo kata ya Sedeko wilaya  Serengeti mkoani Mara wameiomba serikali pamoja na wadau kuwasaidia  kuwajengea bweni ili kuwalinda watoto wao wasishambuliwe na wanyama  wakati wa kwenda shule na kurejea nyumbani.

ITV imefika katika vijiji hivyo ambavyo  ni Bisarasara Bonchuku ,Sedeko na Nyamburi ambavyo viko mpakani mwa Hifadhi ya Serengeti na kushuhudia wananchi hao wakiwa wamejenga madarasa nane, maabara mbili na majengo mawili ya utawala kwa garama ya zaidi ya shilingi milioni mia mbili kwa nguvu zao. 

Wananchi hao wameungana kwa pamoja  na kuchangishana fedha kupitia makundi rika na wadau mbalimbali na kujenga shule  mbili ndani ya kata moja ambazo ni Sedeko na Nyamburi.