Back to top

Wananchi wachanga fedha na kutengeneza kivuko cha miti

18 January 2020
Share

Wananchi katika kijiji cha Utengule kata ya Mambwenkoswe wilayani Kalambo mkoani Rukwa wamelazimika kuchangishana fedha na kujenga kivuko cha miti  katika mto  Mlenje baada ya mto huo kujaa maji wakati wa masika na kusababisha wanafunzi pamoja na wakazi wengine kushindwa kuvuka na hivyo  kukatika kwa mawasiliano na kuiomba serikali kupitia wakala wa barabara vijijini na mijini TARURA kujenga daraja la kudumu.

Wakiongea katika  nyakati tofauti, wananchi  kijijini  hapo wamesema serikali  haina budi kuwasaidia kujenga kivuko imara kwani kilichopo si salama kwa maisha yao kutokana na kujengwa kwa miti ambapo mwaka jana serikali ya kijiji husika ililazimika kuifunga shule ya msingi ili kuokoa maisha ya watoto.

Meneja wa barabara za vijijini na mijini TARURA wilayani  Kalambo Japhet  Elvas, amesema  serikali  imetenga  bajeti  kwa mwaka 2020 /21 kwa ajili  ya  ujenzi  kwa   kivuko  hicho na kuwasihi wananchi kuwa wavumilivu wakati suala lao  likishughulikiwa na huku kaimu mkurungezi wa  halmashauri hiyo Magreth  Kakoyo akiwataka  wananchi kuwa  makini  na watoto  wao  ili  wasivuke  kwenye  mto huo  pindi maji  yanapojaa.