Back to top

Wananchi walalamikia ubovu wa stendi kuu ya mabasi Songea

09 February 2019
Share

Wananchi wa manispaa ya Songea mkoani Ruvuma wamelalamikia ubovu  wa stendi kuu ya mabasi  ya Msamala  wilayani Songea  ambapo  wameiomba serikali kutengeneza stendi hiyo na kuwaondolea adha wananchi.

Wananchi  wakiwemo madereva na makondakta ambao magari yao yanapitia katika kituo kikuu  hicho cha  mabasi yaendayo mikoani wanasema kutokana na mashimo katika stendi hiyo na ubovu wa  barabara za kuingilia stendi magari yao yamekuwa yakiharibika
Kwa aupande wao abiria wanasema kuwa uchafu katika stendi hiyo ni changamoto nyingine na pia vyoo havitoshelezi.

Akijibu malalamiko hayo mkurugenzi mtendaji wa manispaa ya Songea  Bi.Tina Sekambo amekiri kituo hicho cha  mabasi  Songea kukabiliwa na changamoto lukuki na kwamba wametenga milioni 70 za ukarabati.