Back to top

Wanaodaiwa kufukiwa na kifusi North Mara, kukamatwa wakipatikana.

20 February 2021
Share

Serikali mkoani Mara imesema bado inaendelea na uchunguzi wa kuwasaka watu saba wanaodaiwa kufukiwa na kifusi  ndani ya mgodi wa North Mara Nyamongo na  kudai wakipatikana watakamatwa kwani ni wahalifu kama walivyo wahalifu wengine.
.
Mkuu wa mkoa wa Mara Adam Malima ameyasema hayo kufuatia tetesi juu ya watu saba wanaodaiwa kuingia ndani ya mgodi wa North Mara kwa madai yakwenda kuiba dhahabu.