Back to top

YANGA KUZINDUA DOCUMENTARY, KAMA USHAHIDI KWA VIZAZI VIJAVYO

03 August 2023
Share

Timu ya soka ya Yanga SC imetangaza kuzindua Documentary itakayoelezea mafanikio ya timu hiyo katika msimu wa mwaka 2022/23, siku ya jumatatu, ya Agosti 7, 2023, katika ukumbi wa sinema wa Century Cinemax, uliopo Dar Free Market, mkoani Dar es Salaam.
.
Akitoa taarifa hiyo Afisa Habari wa timu hiyo Bw.Ally Kamwe, amebainisha kuwa Documentary hiyo itakuwa na kila taarifa na tukio, lililotokea kwenye timu hiyo katika msimu wa mwaka 2022/23.


Kamwe amebainisha kuwa lengo la timu hiyo kuzindua Documentary hiyo, ni kuhakikisha vizazi vijavyo vinakuwa na ushahidi kuwa timu hiyo iliwahi kushiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.