Back to top

YANGA NA SIMBA KUKUTANA APRILI 20, KWA MKAPA

07 April 2024
Share

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imetangaza tarehe ya mchezo, utakaowakutanisha watani wa jadi, Young Africans na klabu ya Simba (Kariakoo Derby).
.
Mchezo huo ambao ulikuwa haujapangiwa tarehe kwenye ratiba iliyofanyiwa maboresho na kutangazwa Februari 2024, sasa utachezwa kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa, siku ya Jumamosi, Aprili 20, 2024, saa 11:00 jioni.