
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imewahakikisha wananchi kuwa Zanzibar itafuata sheria na serikali haitokubali kuona Zanzibar ndio dampo la vyakula na dawa zisizofaa kwa matumizi ya binadamu.
Msimamo huo umetolewa na waziri wa afya wa Zanzibar Mhe. Hamad Rashid Mohamed katika hotuba yake iliyosomwa na naibu waziri wa afya Mhe. Harusi katika uzinduzi wa Zanzibar kujiunga kimataifa na mfumo wa TEHAMA wa ukaguzi na uingizaji wa vyakula na dawa nchini ambapo kupitia wakala wa vyakula na dawa Zanzibar inakuwa nchi ya tano katika ukanda wa Afrika Mashariki ambapo Mhe. Waziri amesema serikali imepania kuona vyakula na dawa zinazoingia zimedhibitiwa na wakala na kusajiliwa ndani na nje.
Mapema mkurengezi mtendaji wa wakala wa vyakula na dawa Zanzibar Dkt. Burhan Simai amesema kuanza kwa mfumo huo utaleta mabadiliko makubwa Zanzibar kwa jamii ikiwa ni pamoja kuhakikishiwa vyakula na dawa zinatambulika na huduma kupatikana kwa muda mfupi,huku mkurugenzi wa TRADEMARK East Africa John Ulanga ambao ndio wafadhili na wasimamizi wakuu wa mradi huo,amesema tasisi hiyo itaendelea kuona ushindani wa kibiashara wenye tija unaendelezwa.
Uzinduzi huo uliohudhuriwa na wadau mbali mbali wa taassi za serikali za huduma za vyakula na dawa na pia wafanyabishara unaifanya Zanzibar kuungana kimatifa na Tanzania bara, Kenya ,Uganda na Rwanda.