
Shughuli za utalii katika hifadhi ya taifa ya ziwa Manyara zilizokuwa zimesimama kwa muda baada ya miundombinu ya barabara kuathiriwa na mvua sasa zimenaendelea baada ya maeneo yaliyokuwa yameharibiwa na mafuriko kutengenezwa.
Meneja mahusiano wa shirika la hifadhi za taifa Tanzania (TANAPA) Bw.Pascal Shelutete amesema pamoja na hatua hiyo shirika limechukua tahadhari katika hifadhi zote 16 ya kukabiliana na athari za mvua na kuhakikisha kuwa shughuli za utalii zinaendelea kama kawaida na kwamba shirika litahakikihsa wageni wote wanaendelea na safari zao kama kawaida.
Hifadhi ya taifa ya ziwa Manyara ni miongoni mwa zilizokuwa zimeathiriwa na mvua zinazoendelea ambazo licha ya kuzoa daraja muhimu katika barabara inayoingia katika hifadhi hiyo ziliharibu mioundombinu katika maeneo mbalimbali ya hifadhi hiyo na pia hifadhi zingine.
.............