
Watumiaji wa barabara ya siwa iliyopo Mikocheni viwandani kupitia kituo cha utangazaji cha ITV wamesema mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam zimesababisha baadhi ya sehemu za barabara hiyo kuendelea kuchimbika na idadi ya madimbwi kuongezeka na kushindwa kupitika kwa urahisi huku Mhandisi Daud Sigalla kutoka TARURA akiahidi kuwa wanaendelea na mazungumzo na mkandarasi wa awali na kazi ya ujenzi itaanza muda wowote.