
Zaidi ya hekta Elfu ishirini sawa na ekari elfu hamsini za mashamba ya mahindi ya wakulima wadogo katika vijiji vya wilaya ya Mvomero zimeteketezwa kwa kuliwa na wadudu waharibifu wa mimea aina ya Viwavi Jeshi vamizi Fall Armyworm.
Baadhi ya wakulima ambao mashamba yao yamevamiwa na Viwavi Jeshi vamizi wanasema wamepata hasara kubwa katika msimu huu wa kilimo hali iliyowakatisha tamaa ya kuendelea na shughuli ya kilimo .
Afisa Kilimo Umwagiliaji na Ushirika wilaya ya Mvomero Daina Mnywanga anasema tatizo ni kubwa.
Baada ya kutembelea eneo lililoathirika na kutoa elimu kwa waafisa ugani wakulima pamoja na wakala wa pembejeo za kilimo mtafiti wa wadudu waharibifu na viutilifu kutoka TPRI anasema hadi sasa zaidi ya mikoa kumi na sita imesha athirika na wadudu hao na kwamba tpri imeshapata viuatilifu vyenye uwezo wa kuua wadudu hao na wanaendelea kutoka elimu.