
Rais wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Amina Suleiman Msengwa kuwa Mwenyekiti wa
Bodi ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS).
Dkt. Msengwa ni Mhadhiri na Mkuu wa Idara ya Takwimu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Dkt.Msengwa amechukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Andrew Massawe ambaye amemaliza muda wake.
Taarifa iliyolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Mhe. Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi huu umeanza tarehe 19 Septemba, 2019.