
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Philip Mpango ameagiza watumishi wa sekta ya afya katika zahanati, vituo vya afya na hospitali watakaobainika kushiriki katika wizi wa dawa za serikali waondolewe kazini mara moja .
Akizungumza na wakazi wa kata ya Bagara mkoani Manyara Dk.Philip Mpango amesema kuwa serikali haitawavulimia watumishi wa sekta ya afya wanaoiba dawa za serikali.
kwa upande wake Naibu Waziri wa TAMISEMI David Silinde amesema kuwa serikali itahakikisha upatikanaji wa dawa pamoja na kudhibiti upotevu wa dawa.
