
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Dkt. John Jingu amewataka wakandarasi wanaojenga majengo ya Wizara Awamu ya Pili katika Mji wa Serikali Mtumba, Jijini Dodoma kuongeza kasi ya ujenzi ili kumaliza kwa wakati.
.
Dkt.Jingu alitoa kauli hiyo Jijini Dodoma alipofanya ziara yake kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi huo ambapo alisema ujenzi unaendelea vizuri huku akiwahimiza kuongeza wafanyakazi.

Aidha, Dkt.Jingu aliwaagiza kuongeza muda wa kazi na kuongeza vifaa hatua itakayorahisisha kazi hiyo kufanyika kwa kasi inayotarajiwa ili ofisi hizo kuanza kutumika mara moja akisema kulingana na hali ya ujenzi baadhi ya majengo yatamalizika kabla ya muda uliopangwa.
.
“Kwa ujumla ni kwamba ujenzi unaenda vizuri ushauri mkubwa ni tuongeze kasi ya utendaji kazi na hasa kununua mahitaji ya vifaa kwa ujumla na wafanyakazi waongezwe itaweza kusaidia kwenda kwa kasi ambayo viongozi wetu Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, Mhe. Waziri MKuu Kassim Majaliwa na viongozi wengine wanatarajia,” alisema Dkt. Jingu.
