Back to top

TRA: kodi ya pango ya 10% sio mpya

26 August 2022
Share

Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imesema kuwa kodi ya pango inayotokana na mapato ya pango la nyumba kwa 10% sio mpya bali wigo umeongezwa ili wapangishaji wa nyumba binafsi kama ilivyokuwa kwa wenye nyumba za biashara nao wamejumuishwa kwenye wigo wa kodi kuanzia Julai 01, 2022.
.
Aidha Mamalaka hiyo imebainisha kuwa mwenye nyumba atapata cheti cha kodi ya zuio kama ushahidi wa malipo ya kodi iliyolipwa.