
Mwanafunzi wa darasa la saba (17) katika shule ya msingi Mbuza, Kata ya mkoe Wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa, amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuozeshwa kwa nguvu na wazazi wake wakati wa kipindi cha likizo Juni 2023, hali iliosababisha kushindwa kuendelea na masomo yake.
Kutokana na sakata hilui viongozi wa serikali ya Kijiji hicho akiwemo Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Alisen Machenchewa na Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Mbuza, Fidelsi Mbuluko, wamesema baada ya mwanafunzi kutoonekana shule tangu kufunguliwa, waliamua kuanzisha msako wa nyumba kwa nyumba na kukuta akiwa ameozeshwa na wazazi wake.
