Back to top

Mason kuendelea kushikiliwa kwa unyanyasaji wa kingono.

02 February 2022
Share

Mchezaji wa soka wa Manchester United Mason Greenwood (20) aliyekamatwa siku ya Jumapili kwa tuhuma za ubakaji na shambulio ataendelea kuwekwa kizuizini kufuatia tuhuma zinazomkabili za unyanyasaji wa kingono na kutoa vitisho vya kuua.

Polisi wa Greater Manchester (GMP) walisema wamepewa muda zaidi wa kumhoji baada ya kuongezewa muda hapo awali hadi Jumatatu.

Manchester United imesema hatachezea klabu hiyo hadi itakapotangazwa tena.