
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, ametembelea na kukagua mradi wa Ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) Mwanza-Isaka, ambao umefikia 28.03%, ambapo amesema amefurahishwa na maendeleo ya ujenzi wa mradi huo huku akitoa wito kwa wananchi wa maeneo hayo kuwa walinzi wa vifaa na mitambo inayotumika katika ujenzi huo.
.
Mradi huo wenye jumla ya kilometa 341, ambao hadi kukamilika kwake utagharimu shilingi Tril. 3.062, umetoa ajira zaidi ya 6,720 na kandarasi ndogo zenye thamani ya shilingi Bil. 80 hadi sasa.
