Back to top

Mapato: Kibaha yaongoza, Bumbuli yavuta mkia

02 August 2022
Share

Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha,  imeongoza katika ukusanyaji wa mapato,  ambapo imekusanya asilimia  247 ya makisio yake ya mwaka, ikifuatiwa na Halmashauri za Wilaya ya Mlele 185%, na Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro 158% , huku Halmashauri ya Wilaya ya Bumbuli ikiwa ya mwisho kwa kukusanya 58% ya makisio yake ya mwaka, ikifuatiwa na Halmashauri za Wilaya ya Korogwe 67% na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda 70%.
.
Hayo yamesemwa na Waziri wa TAMISEMI, Mhe.Innocent Bashungwa , wakati akitoa taarifa kuhusu mapato na matumizi ya ndani ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2021/2022 ambapo amebainisha kuwa Halmashauri 100 zimekusanya mapato ya ndani kwa asilimia 100 au zaidi ya lengo la mwaka.